Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb), akizungumza na Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Maji Tanzania Bara jijini Dodoma
08 May, 2026
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb), akizungumza na Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Maji Tanzania Bara jijini Dodoma kuelekea utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/27.
Waziri Aweso amesisitiza uwajibikaji, ufanisi na usimamizi madhubuti wa miradi ya maji kwa kuzingatia manufaa ya wananchi.
Amewataka watendaji hao kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na ushirikiano ili kuendelea kuisogeza mbele Sekta ya Maji nchini sambamba na kutekeleza maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu ya maji.

